Matthew 27:57-61

57 aIlipofika jioni, alifika mtu mmoja tajiri kutoka Arimathaya aitwaye Yusufu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Isa. 58Akamwendea Pilato ili kumwomba mwili wa Isa. Pilato akaamuru apewe. 59Yusufu akauchukua mwili wa Isa, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, 60 bna kuuweka katika kaburi lake mwenyewe jipya, alilokuwa amelichonga kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa katika ingilio la kaburi, akaenda zake. 61Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwepo mahali pale, wakiwa wameketi mkabala na kaburi.

Walinzi Pale Kaburini

Copyright information for SwhKC